Tuesday, September 29, 2015

WENGER AMTAKA CHAMBERLAIN KUJIFUNZA KUTOKA KWA SANCHEZ.

MENEJA wa Arsenal, Arsene Wenger amesema Alex Oxlade-Chamberlain anaweza kujifunza kutoka kwa mchezaji mwenzake Alex Sanchez jinsi ya kujiweka katika nafasi nzuri ili aweze kupata kufunga mabao. Nyota huyo wa kimataifa wa Chile ambaye amejiunga na Arsenal akitokea Barcelona msimu uliopita alifunga hat0trick katika ushindi wa mabao 5-2 waliopata dhidi ya Leicester City Jumamosi iliyopita. Sanchez alianza msimu wake wa kwanza vyema akiwa na Arsenal kwa kufunga mabao 25 katika mechi 52 alizocheza na kuisaidia timu hiyo kutetea taji lake la Kombe la FA. Oxlade-Chamberlin huu ni msimu wake wa tano akiwa na klabu hiyo ambapo ameambulia kufunga mabao 13 katika mechi 126 alizocheza. Hata hivyo Wenger ana imani kuwa nyota huyo wa kimataifa wa Uingereza anaweza kuongeza kasi ya ufungaji pindi atakapojifunga kupokea mipira katika eneo la hatari.

No comments:

Post a Comment