Tuesday, September 29, 2015

UKATA WANUKIA WOLFSBURG BAADA YA WADHAMINI WAO VOLKSWAGEN KUBAMBWA KWA UDANGANYIFU.

KLABU ya Wolfsburg ya Ujerumani inaweza kukabiliwa na matatizo ya kifedha siku za usoni kwasababu ya ya kashfa ya inayowakabili wadhamini wao kampuni ya Volkswagen. Kampuni ya kutengeneza magari ya Kijerumani inaweza kukabiliwa na faini ya zaidi ya paundi bilioni 11.8 baada ya kukwepa majaribio ya kupima ubora wake nchini Marekani. Taarifa hizo zinakuja wakati Wolfsburg wakikabiliwa na mchezo muhimu wa Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Manchester United kesho. Wataalamu wa masuala ya uchumi wametabiri kuwa klabu hiyo lazima itakumbwa na msukosuko wa kiuchumi kama kampuni hiyo ikilimwa faini hiyo kwani itabidi wapunguze matumizi ili kukabiliana na hali halisi na masuala ya udhamini ndio jambo la kwanza kuangaliwa.

No comments:

Post a Comment