Wednesday, September 30, 2015

BARCELONA YAZIDI KUANDAMWA NA MAJERUHI.

MATATIZO ya majeruhi yameendelea kuiandama Barcelona kufuatia nahodha wake Andres Iniesta kutolewa nje katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Bayer Leverkusen jana kutokana na kusumbuliwa na msuli wa paja. Nafasi ya Iniesta ilichukuliwa na Jordi Alba wakati Barcelona wakiwa nyuma kwa bao 1-0 lakini mabao mawili yaliyofungwa katika dakika 10 za mwisho na Sergio Roberto na Luis Suarez yalitosha kuwapa ushindi wa mabao 2-1. Mabingwa hao wa Ulaya tayari wanamkosa nyota wao mshindi wa tuzo nne za Ballon d’Or Lionel Messi ambaye amajeruhi yatamuweka nje kwa muda wa miezi miwili. Barcelona walikataa kutaja muda halisi ambao Iniesta anaweza kukaa nje lakini tetesi zinadai kuwa wanaweza kumkosa kwa muda wa mwezi mmoja.

No comments:

Post a Comment