Wednesday, September 30, 2015

ROSSI AKUBALI KULIMWA MSHAHARA FIORENTINA.

WAKALA wa mshambuliaji Giuseppe Rossi amedai kuwa mteja wake ameonyesha mapenzi na uaminifu kwa klabu ya Fiorentina baada ya kukubali kupunguziwa mshahara wake. Nyota huyo aliyekuwa akisumbuliwa na majeruhi ambaye amerejea hivi karibuni baada ya miezi 15 ya kujiuguza, amekubali kupunguziwa mshahara wake katika kipindi hiki ambacho anapambana kurejea katika ubora wake. Mkataba wa nyota huyo wa kimataifa wa Italia ambao aliusaini wakati akijiunga na klabu hiyo mwaka 2013 bado unatarajiwa kumalizika katika msimu wa 2016-2017. Wakala huyo Andrea Pastorello amesema kitendo cha Rossi kukubali kupunguza mshahara wake bila kushurutishwa ni kuonyesha makubwa aliyonayo kwa klabu na mashabiki wake kwa ujumla. Rossi ameshaitumikia Fiorentina katika michezo miwili msimu huu mpaka hivi sasa.

No comments:

Post a Comment