Wednesday, September 30, 2015

KHEDIRA FITI KUIVAA SEVILLA.

KIUNGO mahiri wa kimataifa wa Ujerumani, Sami Khedira anatarajiwa kuanza kuitumikia kwa mara ya kwanza Juventus katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Sevilla baadae leo. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 28 alipata majeruhi ya misuli katika mchezo wa kirafiki kujiandaa na msimu mpya dhidi ya Marseille Agosti lakini sasa amerejea kuwa miongoni mwa wachezaji wa kikosi cha kwanza. Akihojiwa meneja wa Juventus, Massimiliano Allegri amesema hakuna shaka kuwa Khedira atakuwepo katika mchezo huo kwani amekuwa akifanya mazoezi vyema na wenzake. Pamoja na kusuasua katika Serie A Juventus walianza vyema katika michuano hiyo baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 katika mchezo wao wa kwanza dhidi ya Manchester City.

No comments:

Post a Comment