Wednesday, September 30, 2015

KLOPP ACHOMOA KUINOA MEXICO.

KATIBU mkuu wa Shirikisho la Soka la Mexico, Guillermo Cantu amethibitisha kuwa shirikisho lilimfuata meneja wa Borussia Dortmund Jurgen Klopp kuchukua mikoba ya kuinoa timu ya taifa ya nchi hiyo. Klopp aliondoka Dortmund kufuatia msimu usioridhisha wa 2014-2015 ambapo klabu hiyo ilikosa nafasi ya kufuzu michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya na amekuwa akihusishwa na tetesi za kwenda kuinoa Liverpool pindi Brendan Rodgers muda wake utakapokwisha Anfield. Cantu amesema walizungumza na wawakilishi wake lakini waliwajibu kuwa kwasasa yuko mapumzikoni hivyo haitawezekana kukubali kuchukua mikoba ya kuinoa nchi hiyo. Hata hivyo, Cantu aliendelea kudai kuwa Klopp alikuwa katika mipango yao ya muda mfupi kwasababu hana ujuzi na soka la Mexico na hazungumzi Kihispania.

No comments:

Post a Comment