Wednesday, September 30, 2015

MOURINHO AWALAUMU WACHEZAJI WAKE KWA KUKUBALI KUFUNGWA MABAO YA KIJINGA.

MENEJA wa Chelsea Jose Mourinho amelaumu nyakati mbili za kijinga baada ya kikosi chake kupoteza mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya FC Porto. Chelsea walipokea kipondo cha tano msimu huu katika mashindano yote baada ya kukubali kufungwa mabao 2-1 na Porto. Akihojiwa mara baada ya mchezo huo, Mourinho amesema wametizama mara kadhaa jinsi Porto wanavyopiga kona zao na walikuwa wako tayari kwa hilo. Chelsea sasa wanakuwa wamepoteza michezo mingi zaidi msimu huu kuliko msimu wote wa 2014-2015ambao walipoteza michezo minne pekee. Mourinho aliendelea kudai kuwa anaamini walifanikiwa kumudu mchezo huo lakini walikubali kufungwa mabao ya kijinga jambo lililowagharimu kupoteza mchezo huo. Chelsea wanashika nafasi ya tatu katika kundi G wakiwa nyuma ya Porto na Dynamo Kiev kwa alama moja.

No comments:

Post a Comment