Wednesday, September 30, 2015

LEWANDOWSKI NA UCHU WA KUFUNGA MABAO.

MSHAMBULIAJI wa Bayern Munich Robert Lewandowski amesisitiza kuwa hajaridhishwa na idadi ya mabao aliyofunga katika wiki za karibuni na anataka kuendelea wimbi hilo la ufungaji zaidi katika wiki zijazo. Nyota huyo wa kimataifa wa Poland alifunga hat-trick katika ushindi wa mabao 5-0 waliopata Bayern dhidi ya Dinamo Zagreb jana katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya na kufanya kufikisha idadi ya mabao 14 katika mechi 10 alizocheza za mashindano yote msimu huu. Akihojiwa Lewandowski amesema haijalishi amefunga mabao mangapi lakini uchu wake yeye ni kufunga mabao mengi zaidi. Nyota huyo aliendelea kudai kuwa kuna nafasi kadhaa alipata ambazo zilikuwa za kufunga lakini hakufunga na hiyo inaonyesha ni jinsi anavyotakiwa kuendelea kujituma ili aweze kutumia kila nafasi anayopata.

No comments:

Post a Comment