Wednesday, September 30, 2015

WENGER AJIPA MATUMAINI.

MENEJA wa Arsenal, Arsene Wenger amesisitiza kikosi chake bado kinaweza kufuzu hatua ya timu 16 bora za michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya pamoja na kuburuza mkia katika kundi F wakiwa hawajaambulia alama yeyote. Arsenal jana walikubali kipigo cha pili mfululizo katika michuano hiyo baada ya kufungwa na Olympiakos kwa mabao 3-2 katika mchezo uliofanyika katika Uwanja wa Emirates huku wakikabiliwa na mechi zingine mbili ngumu dhidi ya Bayern Munich. Akihojiwa Wenger amesema matokeo hayo yamewaacha katika nafasi mbaya lakini bado anaamini wanaweza kufuzu hatua inayofuata. Kocha huyo aliendelea kudai kuwa wanachotakiwa kufanya hivi sasa ni kuhakikisha wanapata matokeo mazuri katika mechi zao zinazofuata dhidi ya bayern.

No comments:

Post a Comment