Wednesday, September 30, 2015

PLATINI ASISITIZA KUENDELEA KUGOMBEA URAIS FIFA PAMOJA NA KUCHUNGUZWA.

WAENDESHA mashitaka nchini Uswisi wamedai kuwa rais wa Shirikisho la Soka la Ulaya-UEFA Michel Platini anatumiwa kama shahidi na mtuhumiwa katika uchunguzi wa masuala ya rushwa katika Shirikisho la Soka Duniani-FIFA. Waendesha mashitaka hao wanamtuhumu rais wa FIFA Sepp Blatter kulipa malipo yasiyo halali ya dola milioni 2 kwa Platini. Platini amewasilisha maelezo katika uchunguzi huo lakini amesema amefanya hivyo kama shahidi huku wote wawili wakikabusha kufanya jambo lolote baya. Platini amesema bado anataka kuendelea na harakati zake za kugombani urais wa FIFA pindi Blatter atakapoachia ngazi. Hata hivyo mwanasheria mkuu wa Uswisi Michael Lauber amesema hakumuhoji Platini kama shahidi kwani naye pia ni mtuhumiwa naayefanyiwa uchunguzi katika sakata hilo.

No comments:

Post a Comment