Friday, October 16, 2015

ALABA AMTABIRIA MAKUBWA LEWANDOWSKI.

BEKI wa Bayern Munich, David Alaba amedai kuwa Robert Lewandowski anaweza kufikia rekodi ya Bundesliga iliyowekwa na Thomas Mueller mwaka 1972 kwa kufunga mabao 40 kwa msimu. Nyota huyo wa kimataifa wa Poland amekuwa katika kiwango bora msimu huu akiwa ameshafunga mabao 12 katika mechi nane za ligi walizocheza yakiwemo na mabao matano aliyofunga ndani ya dakika tisa katika mchezo dhidi ya Wolfsburg mwezi uliopita. Bayern ambao wameshinda mechi zao zote nane za walizocheza na kuongoza Bundesliga kwa tofauti ya alama saba dhidi ya Borussia Dortmund, watasafiri mwishoni mwa wiki hii kuifuata Werder Bremen. Akizungumza na wanahabari Alaba amesema mabao 40 yanaweza kuonekana mengi lakini kila kitu kinawezekana kwa Lewandowski.

No comments:

Post a Comment