Friday, October 16, 2015

BABA YAKE NEYMAR ATHIBITISHA MAN UNITED KUMTAKA MWANAE.

BABA wa mshambuliaji nyota wa Barcelona Neymar amethibitisha kuwa Manchester United walijaribu kutaka kumshawishi aende Ligi Kuu lakini walikataliwa ofa yao. Nahodha huyo wa kimataifa wa Brazil kwasasa yuko katika mzungumzo na kusaini mkataba mpya wa muda mrefu huku makubaliano ya mwisho yakitarajiwa kuwa mwanzoni mwa mwakani. Lakini jana jioni, baba wa nyota huyo ambaye pia ndio wakala wake alibainisha kuwa tetesi ambazo zinavuma kuwa United iliwahi kutaka kumsajili mwanae ni kweli. Mzee huyo aitwaye Neymar Sr amesema ni kweli ofa ya United ilifika Barcelona na klabu iliwasiliana nao wakiwaambia kuwa hawana mpango wa kumuuza. Neymar Sr aliendelea kudai kuwa klabu iliwauliza kama wanaitaka lakini hilo halikuwa tatizo kwani Barcelona wasingemwachia kwasababu alikuwa bado ana mkataba wa miaka mitatu.

No comments:

Post a Comment