Friday, October 16, 2015

MOURINHO KUPINGA ADHABU YA FA.

MENEJA wa Chelsea, Jose Mourinho anatarajia kukata rufani kupinga adhabu aliyopewa na Chama cha Soka cha Uingereza-FA ya kufungiwa mechi moja na faini ya paundi 50,000 kwa kauli yake dhidi ya mwamuzi aliyechezesha mchezo kati ya timu yake na Southampton. Mourinho anayefahamika kwa kauli zake zenye utata, alilimwa adhabu hiyo kufuatia kumtuhumu mwamuzi kwa kuwanyima penati kutoka uoga katika mchezo ho ambao walitandikwa mabao 3-1 katika Uwanja wa Stamford Bridge. Lakini akizungumza na wanahabari leo kuelekea katika mchezo wao wa keshi dhidi ya Aston Villa, Mourinho aliwahakikishia kuwa atapambana kupinga adhabu hiyo. Mourinho amesema anataka kuwa mkweli mwake mwenyewe hilo ndio jambo la muhimu hivyo atakata rufani kupinga adhabu hiyo. Kocha huyo pia alikiri kuwa tabia yake inaweza kumpa wakati mgumu siku moja kuja kuinoa timu ya taifa ya Uingereza chini ya chama hicho.

No comments:

Post a Comment