Friday, October 16, 2015

ROONEY FITI KUIVAA EVERTON.

MSHAMBULIAJI wa Manchester United, Wayne Rooney amefaulu vipimo vya afya kwa ajili ya mchezo wa Ligi Kuu dhidi ya Everton kesho. Nahodha huyo wa United alizikosa mechi za kufuzu michuano ya Euro 2016 dhidi ya Estonia na Lithuania kutokana na majeruhi ya kifundo cha mguu aliyopata katika mchezo waliotandikwa mabao 3-0 na Arsenal kabla ya mapumziko ya mechi za kimataifa. Hata hivyo, sasa United imethibitisha nyota huyo mwenye umri wa miaka 29 yuko fiti na atakuwepo katika mchezo huo dhidi ya Everton. Beki Michael Carrick naye pia ameruhusiwa kucheza baada ya kukosa mechi zote za kimataifa za Uingereza kutokana na majeruhi ya nyonga. Marco Rojo aliyekuwa akisumbuliwa na msuli wa paja na Ander Herrera wote wamepimwa na kuonekana kuwa fiti kwa ajili ya mchezo huo ingawa wanaweza wasicheza dakika zote 90.

No comments:

Post a Comment