Friday, October 16, 2015

YAYA TOURE, NASRI WAREJEA KIKOSI CHA CITY.

MENEJA wa Manchester City, Manuel Pellegrini amesema Yaya Toure na Samir Nasri wote wako fiti kwa ajili ya mchezo wa kesho wa Ligi Kuu dhidi ya Bournemouth. Viungo hao walikuwa wakisumbuliwa na majeruhi ya msuli wa paja hatua iliyowakosesha mchezo wa ligi dhidi ya Newcastle United ambao walishinda kwa mabao 6-1 lakini sasa wanaonekana kuwa fiti tayari kwa kesho. Pellegrini alithibitisha taarifa hizo lakini kwa Fabian Delph amesema atahitaji wiki moja zaidi ya kujiuguza kabla ya kurejea uwanjani. Meneja huyo aliendelea kudai kuwa majeruhi aliyopata Sergio Aguero katika mechi za kimataifa hadhani kama ataweza kurejea uwanjani kabla ya mwezi mmoja.

No comments:

Post a Comment