Tuesday, October 27, 2015

ALLEGRI ATETEA UAMUZI WAKE WA KUMUWEKA BENCHI DYBALA.

MENEJA wa Juventus, Massimiliano Allegri ametetea uamuzi wake wa kutomtumia Paulo Dybala alisajiliwa kwa fedha nyingi wiki iliyopita baada ya kukosolewa na rais wa Palermo Maurizio Zamparini. Zamparini alimtuhuma Allegri kwa kumharibia Dybala kiwango chake baada ya kumchezesha kwa dakika tisa katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Borussia Manchengladbach wiki iliyopita. Akizungumza na wanahabari kuelekea mchezo wao wa kesho dhidi ya Sassoulo, Allegri amesisitiza uchaguzi wa kikosi chake hutegemea kiwango cha wachezaji. Kocha huyo amesema yeye huwa hachagui wachezaji kutokana na fedha walizogharimu, huwa anachagua wachezaji wanaocheza vyema.

No comments:

Post a Comment