Tuesday, October 27, 2015

LUIS ENQRIQUE KUWAPUMZISHA SUAREZ NA NEYMAR KESHO.

MENEJA wa Barcelona, Luis Enrique amewaacha Luis Suarez na Neymar katika kikosi chake cha wachezaji 16 watakaocheza mchezo wa Kombe la Mfalme dhidi ya Villanovense. Barcelona itasafiri kwenda Extremadura kukwaana na timu hiyo ya daraja la pili kesho bila nyota wake hao pamoja na Lionel Messi aliyekuwa majeruhi. Hata hivyo, kocha huyo amekiri ana matumaini kuwa ataweza kuondoka na wachezaji wengi zaidi wa kikosi cha kwanza. Nyota wengine walioachwa ni pamoja na Sergio Busquets, Javier Marcherano, Gerard Pique na Claudio Bravo wakati Andres Iniesta yeye akiwa bado hajapona sawaswa majeruhi ya msuli wa paja yanayomsumbua.

No comments:

Post a Comment