Friday, October 30, 2015

MAKOCHA WAJIUZULU ARGENTINA.

MAKOCHA wawili Edgardo Bauza wa klabu ya San Lorenzo na Diego Cocca wa Racing ambao waliziongoza timu zao kushinda mataji makubwa mwaka jana, wametangaza kujiuzulu nyadhfa zao hizo wakati msimu wa Ligi Kuu nchini humo utakapomalizika mwezi ujao.  Bauza aliiongoza Lorenzo kunyakuwa taji lao la kwanza la Kombe la Libertadores la Amerika Kusini mwaka jana kabla ya Cocca kuingoza Racing ksushinda taji la ligi kwa mara ya kwanza baada ya miaka 13. Akihojiwa Bauza amesema yeye pamoja na wasaidizi wake wameamua kuachia ngazi na kuondoka kwani wameona ni jambo zuri kwa klabu na timu. Naye Cocca akizungumza na wanahabari alitangaza taarifa kama hizo za kuondoka mwishoni mwa msimu lakini alikanusha kama kuondoka kwake kunahusiana na masuala ya maslahi.

No comments:

Post a Comment