Friday, October 30, 2015

REMY AMPIGIA DEBE MOURINHO ABAKIE CHELSEA.

MSHAMBULIAJI nyota wa Chelsea, Loic Remy amesisitiza kuwa bado anaona meneja wao Jose Mourinho ndio mtu sahihi wa kuendelea kuinoa klabu hiyo. Miezi mitano baada ya kuiongoza Chelsea kunyakuwa taji la Ligi Kuu, Mourinho amekuwa akipambana kutetea kibarua chake na ratiba ya mechi zinafuatia ikiongeza zaidi shinikizo kwa Mreno huyo. Wakiwa wamefungwa mechi tano kati ya 10 za ligi walizocheza, Chelsea wamejikuta wakiwa katika nafasi ya 15 katika msimamo wakikosa alam tisa kufikia nne bora. Lakini pamoja na taarifa tofauti zilizozagaa zikidai wachezaji kadhaa wamekuwa wakimtaka Mourinho kuondoka, Remy amesema meneja wao huyo bado anaungwa mkono na kikosi chake. Nyota huyo wa kimataifa wa Ufaransa, amesema ni muhimu kwa Mourinho kubakia kwani hawataki kukata tamaa sasa.

No comments:

Post a Comment