Tuesday, October 27, 2015

FA YAMSHITAKI RICHARDS KWA VURUGU.

BEKI wa Aston Villa, Micah Richards amefunguliwa mashitaka ya kinidhamu na Chama cha Soka cha Uingereza-FA. Hatua hiyo imefikiwa baada ya Richards kuzozana na beki wa Swansea City, Federico Fernandez katika mchezo baina yao uliochezwa Jumamosi iliyopita katika Uwanja wa Villa Park. FA ilithibitisha taarifa hizo kupitia mtandao wake huku Richards mwenyewe akipewa mpaka siku ya Alhamisi ya Octoba 29 mwaka huu kujitetea. Katika mchezo huo Villa walifungwa mabao 2-1 na Swansea hata ambayo ilipelekea kocha wake Tim Sherwood kutimuliwa.

No comments:

Post a Comment