Tuesday, October 27, 2015

ROONEY AMMWAGIA SIFA SMALLING.

NAHODHA wa Manchester United, Wayne Rooney amedai kuwa beki Chris Smalling ni miongoni mwa mabeki watatu bora duniani hivi sasa. Smalling ambaye ametoka kuwa mchezaji wa muda na kuwa mchezaji wa kudumu katika kikosi cha kwanza chini meneja Louis van Gaal katika kpindi cha miezi 18 iliyopita, amekuwa katika kiwango bora akicheza mechi zote za United msimu huu. Akihojiwa Rooney alimsifu beki huyo na kudai kuwa ni miongoni mwa mabeki wa kati bora kabisa duniani kwasasa kutokana na kiwango chake. Kauli hiyo ya Rooney imekuja kufuatia Van Gaal kudai Smalling mwenye umri wa miaka 25 anaweza kuwa nahodha wa United katika siku za usoni.

No comments:

Post a Comment