Tuesday, October 27, 2015

BARTOMEU AWASHUKIA WANAODAI MESSI ANATAKA KUONDOKA.

RAIS wa Barcelona, Josep Maria Bartomeu amejibu kwa hasira taarifa zinazodai kuwa Lionel Messi ataondoka katika klabu hiyo, akisisitiza kuwa taarifa hiyo ni ya kutia aibu. Nyota huyo wa kimataifa wa Argentina ambaye kwasasa yuko benchi akisumbuliwa na majeruhi ya goti, amekuwa akihusishwa na taarifa za kuondoka huku magazeti yakidai kuwa anaweza kutimkia Ligi Kuu. Akiulizwa suala hilo Bartomeu amesema watu wanaosambaza habari hizo za uongo wanapaswa kuona aibu kwa Messi hana mpango wa kwenda popote. Bartomeu aliendelea kudai kuwa kwasasa Messi anafanya bidii ili aweze kwa fiti kabla ya mchezo wa El Clasico ambao watakwaana na mahasimu wao Real Madrid.

No comments:

Post a Comment