Friday, October 23, 2015

MESSI APIGWA CHINI ORODHA MPYA YA WANAMICHEZO WENYE THAMANI ZAIDI.

MSHAMBULIAJI wa Barcelona, Lionel Messi ameondoshwa katika 10 bora ya orodha ya wanamichezo wenye thamani zaidi duniani. Orodha hizo ambazo hutolewa na gazeti maaruu la Forbes, mwaka 2014 Messi alishika nafasi ya tisa akikadiriwa kuwa na thamani ya dola milioni 12 lakini mwaka huu baada ya kushika kwa thamani ya dola milioni moja, nyota huyo ameondoshwa katika kumi bora. Badala yake mchezaji nyota wa gofu Roy Mcllroy na bondia Floyd Mayweather wameingia katika kumi bora ya orodha hiyo. Nyota wa Real Madrid Cristiano Ronaldo ambaye alikuwa nafasi ya saba mwaka jana naye pia ameshuka kwa nafasi moja mpaka ya nane mwaka huu. 

Orodha kamili ya wanamichezo na thamani zao zilivyoadiriwa ni kama ifiatavyo.

1. Tiger Woods - Worth $30m
2. Phil Mickelson - $28m
3. LeBron James - $27m
- Roger Federer - $27m
5. MS Dhoni - $21m
6. Usain Bolt - $18m
- Kevin Durant - $18m
8. Cristiano Ronaldo - $16m
9. Rory McIlroy - $12m
10. Floyd Mayweather Jr - $11.5m

Orodha ya timu 10 bora za michezo zenye thamani zaidi.
1. New York Yankees - $661m
2. Los Angeles Lakers - $521m
3. Dallas Cowboys - $497m
4. New England Patriots - $465m
5. Real Madrid - $464m
6. Manchester United - $446m
7. Barcelona - $437m
8. Bayern Munich - $375m
9. Los Angeles Dodgers - $373m
10. New York Knicks - $361m

No comments:

Post a Comment