Tuesday, October 27, 2015

TOKYO SEXWALE AJINADI KUIJENGA UPYA FIFA.

MGOMBEA urais wa Shirikisho la Soka Duniani-FIFA, Tokyo Sexwale anataka kulijenga upya shirikisho kwa kurekebisha yale yote mabaya ikiwemo kashfa ya ufisadi inayolikabili hivi sasa. Jumatatu mgombea huyo kutoka Afrika Kusini aliwasilisha maombi yake rasmi ya kugombea nafasi hiyo ya Sepp Blatter ambaye bado anachunguzwa na FIFA kuhusiana na tuhuma za kumlipa fedha Michel Platini bila kufuata utaratibu. Sexwale ambaye ni mfanyabiashara na mfungwa wa zamani wa kisiasa anaungwa mkono na Chama cha Soka cha Afrika Kusini-SAFA na amethibitisha kuwa atasafiri kuelekea jijini Cairo kuomba kuungwa mkono na Shirikisho la Soka la Afrika-CAF. Sexwale ameahidi kuirejesha heshima ya shirikisho hilo kama akishinda uchaguzi huo utakaofanyika Februari mwakani.

No comments:

Post a Comment