Friday, October 30, 2015

SAMATTA, ULIMWENGU KIBARUANI KESHO ALGERIA.

KLABU ya USM Alger ya Algeria kesho itakuwa ikifukuzia taji lake la kwanza la michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika wakati watakapokuwa wenyeji wa TP Mazembe na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo katika mchezo wa fainali ya mkondo wa kwanza. Katika mchezo huo USM itakuwa na kiu na kufikia mafanikio ya wenzao Entente Setif ambao ndio walikuwa mabingwa wa michuano hiyo kwa mwaka jana. Soka la Algeria linaonekana kupata kwa kasi katika miaka ya karibuni kwani kwasasa wao ndio wanaongoza kwa ubora katika orodha za Afrika huku pia wakifanikiwa kutinga hatua ya pili ya michuano ya Kombe la Dunia iliyofanyika mwaka jana. Hata hivyo, USM haitakuwa na kazi rahisi katika mchezo huo kwani Mazembe imejijenga na kuwa timu ya kuogopewa barani Afrika wakiwa wameshinda taji hilo mara nne kati ya sita zilizopita. Mchezo wa mkondo wa kwanza unatarajiwa kuchezwa kesho katika Uwanja wa Omar Hamadi uliopo Algiers na ule wa maruadiano utachezwa jijini Lubumbashi Jumapili ya Novemba 8 mwaka huu. Mshindi wa michuano hiyo ataliwakilisha bara la Afrika katika michuano ya Klabu Bingwa ya Dunia itakayofanyika nchini Japan Desemba mwaka huu.

No comments:

Post a Comment