Friday, October 30, 2015

WENGER ATAMBA PAMOJA NA MSURURU MREFU WA MAJERUHI ALIONAO.

MENEJA wa Arsenal, Arsene Wenger amepuuza tatizo la majeruhi na kusisitiza kuwa atatafuta suluhisho huku wachezaji nane wakikosekana katika kikosi chake. Theo Walcott na Alex Oxlade-Chamberlain nao wameingia katika orodha za majeruhi kufuatia kuumia katika mchezo dhidi ya Sheffield Wednesday, huku Wenger akithibitisha wote watakosekana mpaka baada ya mapumziko kupisha mechi za kimataifa Novemba mwaka huu. Sasa nyota hao wanaungana na Aaron Ramsey, Jack Wilshere, Danny Welbeck, Mikel Arteta, David Ospina na Tomas Rosicky ambao nao wote ni majeruhi. Lakini Wenger amesema ana imani na timu yake ya madaktari na ana uhakika wanaweza kukabiliana na hali hiyo katika mchezo wao dhidi ya Swansea City kesho. Akizungumza na wanahabari Wenger amesema watatafuta suluhisho na anatakiwa kupata suluhisho lenye uhakika.

No comments:

Post a Comment