Tuesday, November 24, 2015

BLATTER, PLATINI WAKABILIWA NA ADHABU YA KUFUNGIWA MIAKA SABA.

RAIS wa Shirikisho la Soka Duniani-FIFA Sepp Blatter na makamu wake Michel Platini ambao wote wamesimamishwa, wanaweza kukabiliwa na adhabu ya kufungiwa miaka saba kama wakikutwa na hatia ya tuhuma za rushwa zinazowakabili. Wachunguzi wa kamati ya maadili ya FIFA kuna uwezekano mkubwa wakapendekeza adhabu juu ya malipo yasiyo ya uaminifu ambayo yalishuhudia Platini akilipwa paundi milioni 1.35 na Blatter. Kulikuwa hakuna mkataba wowote wa maandishi kufafanua malipo hayo ambayo Platini alipokea miaka tisa baadae. Kamati ya uamuzi inatarajiwa kutangaza matokeo ya uchunguzi huo majira ya Christmas. Wawili hao ambao wamesimamishwa kwa siku 90 wamekanusha kufanya jambo lolote baya wakifafanua kuwa malipo hayo yalifanyika kwa kwa kuaminiana kutokana na kazi iliyofanyika.

No comments:

Post a Comment