Thursday, November 26, 2015

DROGBA ATAKA KUINOA CHELSEA.

MSHAMBULIAJI wa zamani wa Chelsea, Didier Drogba amesema wana makubaliano ya kurejea katika klabu hiyo pindi atakapostaafu kucheza na anataka kuwa meneja. Drogba ambaye kwasasa anacheza soka lake nchini Canada, amewahi kufunga mabao 164 katika vipindi viwili tofauti alivyoichezea Chelsea. Akihojiwa Drogba mwenye umri wa miaka 37, amesema anataka kulipa fadhila kwa klabu hiyo ambayo ilimpa vitu vingi jambo ambalo amekubaliana na wakurugenzi. Mkongwe huyo aliendelea kudai kuwa anaweza kurejea klabu hapo kuchukua nafasi yeyote kama mkufunzi wa shule ya michezo ya timu hiyo, mshauri wa safu ya ushambuliaji, mkurugenzi wa michezo au hata meneja. Drogba alifunga penati ya ushindi iliyowapa taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya mwaka 2012 na kushinda taji la nne la Ligi Kuu katika kipindi chake cha pili alichorejea msimu uliopita kabla ya kujiunga na Montreal Impact inayoshiriki Ligi Kuu ya Marekani-MLS.

No comments:

Post a Comment