Monday, November 30, 2015

WAKAZI WA JIJI LA HAMBURG WAGOMA MJI HUO KUANDAA OLIMPIKI.

WAKAZI wa mji wa Hamburg, Ujerumani wamepiga kura ya kukataa mji huo kuwa mwenyeji wa michuano ya Olimpki na Paralimpiki mwaka 2024. Hamburg ulikuwa mmoja kati ya miji mitano iliyobakia katika kinyang’anyiro hicho, wakiwa sambamba na Rome, Paris, Budapest na Los Angeles. Lakini asilimia 51.7 ya wakazi wa mji huo na ule wa jirani wa Kiel ambako ndipo kungefanika mashindano ya maboti, walikataa katika kura za maoni zilizofanyika jana. Maofisa wa Kamati ya Olimpiki ya Ujerumani waliuchagua mji wa Hamburg katika kinyang’anyiro hicho badala ya Berlin. Ujerumani haijaandaa mashindano ya olimpiki toka ile iliyoandaliwa jijini Munich mwaka 1972.

No comments:

Post a Comment