Friday, November 20, 2015

WENGER ATAKA VIPIMO ZAIDI KUNG'AMUA WADANGANYIFU KATIKA SOKA.

MENEJA w Arsenal, Arsene Wenger anataka vipimo bora kwa ajili ya kugundua wachezaji wadanganyifu katika soka na kutaka vipimo vya damu view vikifanyika mara kwa mara. Chama cha Soka Uingereza-FA kilimtaka Wenger mwenye umri wa miaka 66, kufafanua kauli yake aliyotoa kuhusu dawa za kusisimua misuli katika mahojiano na gazeti moja la Ufaransa. Kocha huyo raia wa Ufaransa amesema yuko tayari kuzungumza na FA kwasababu anataka vipimo vifanyike kwa undani zaidi na juu juu kama hivi sasa ili kuweza kulikabili vyema tatizo hilo. Kiungo wa Dinamo Zagreb, Arijan Ademi alishindwa vipimo kufuatia mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya walioshinda dhidi ya Arsenal Septemba mwaka huu. Na Wenger akihojiwa kuelekea mchezo wao wa kesho wa Ligi Kuu dhidi ya West Bromwich Albion, amesema ni ujinga kudhani soka halina masuala ya matumizi ya dawa za kusisimua misuli kama michezo mingine.

No comments:

Post a Comment