Sunday, December 27, 2015

COSTA AMTIA KIWEWE HIDDINK.

MENEJA wa Chelsea, Guus Hiddink amekiri kukosekana kwa Diaego Costa ni pigo kubwa kwa kikosi chao wakati watakapopambana na Manchester United katika Uwanja wa Old Trafford kesho. Hiddink alichukua mikoba ya kuinoa timu hiyo kwa mara ya kwanza toka alipoteuliwa meneja wa muda, akianza sare ya mabao 2-2 waliyopata dhidi ya Watford jana. Matokeo hayo yameifanya Chelsea kuendelea kubaki katika nafasi ya 15 katika msimamo wa ligi na Costa amepata kadi za njano tano kwa msimu huu hivyo atakosa mechi moja mabayo ni dhidi ya United. Akihojiwa Hiddink amesema kumkosa Costa ni pigo kwani amekuwa akiimarika na mchezo wao unaofuata ni muhimu sana kama angekuwepo. Hiddink aliendelea kudai kuwa pamoja na United kusuasua lakini sio timu ya kubeza kwani watakuwa wakicheza kwao.

No comments:

Post a Comment