Thursday, January 28, 2016

ADEBAYOR AANZA JEURI.

MSHAMBULIAJI mpya wa Crystal Palace, Emmanuel Adebayor amekiri kuwa ataifuatilia klabu hiyo zaidi katika Google baada ya kusajiliwa rasmi jana. Nyota huyo wa kimataifa wa Togo alitambulishwa katika klabu hiyo baada ya kusaini mkataba wa kuitumikia mpaka mwishoni mwa msimu huu. Lakini mshambuliaji huyo wa zamani wa Arsenal na Real Madrid ambaye ameondoka Tottenham Hotspurs Septemba mwaka jana, amekiri kuwa hafahamu mengi sana kuhusiana na klabu hiyo. Akihojiwa Adebayor amesema ataingia katika mtandao wa Google ili kufahamu zaidi kuhusu timu hiyo na chochote watakachotaka atawatimizia.

No comments:

Post a Comment