Thursday, January 28, 2016

YABAINIKA MADRID WALIMFUKUZIA MESSI MARA TATU.

KLABU ya Real Madrid ineripotiwa kutaka kumsajili Lionel Messi zaidi ya mara tatu toka mwaka 2011. Taarifa zinadai kuwa Madrid ndio timu iliyowahi kumfuata nyota huyo wa kimataifa wa Argentina mara tatu tofauti lakini mara zote hizo walikataliwa kwani Messi hakuwa na mpango wa kuondoka Barcelona. Mara ya kwanza Madrid kumfuata Messi ilikuwa mwaka 2011 kufuatia klabu hiyo kuhofia Manchester City wanaweza kumshawishi Cristiano Ronaldo kujiunga nao. Majira ya kiangazi mwaka 2013, Madrid kwa mara nyingine tena walihofu Ronaldo anaweza kuondoka na mmoja wa maofisa wake alikwenda kukutana na wawakilishi wa Messi ili kuona uwezekano wa kumsajili. Mara ya mwisho Madrid kutaka kumuwania Messi ilikuwa mwaka mmoja uliopita lakini kama ilivyokuwa huko nyuma, mara hii pia walikataliwa.

No comments:

Post a Comment