Thursday, January 28, 2016

DE BRUYNE AWALAZA MACHO CITY.

MENEJA wa Manchester City, Manuel Pellegrini anafikiri Kevin de Bruyne ataweza kucheza tena msimu huu baada ya kiungo huyo kuumia goti lake la kulia katika mchezo wa nusu fainali ya Kombe Ligi dhidi ya Everton jana. Nyota huyo wa kimataifa wa Ubelgiji mwenye umri wa miaka 24 ambaye alivunja rekodi ya klabu kwa kusajiliwa kwa kitita cha paundi milioni 55, alipata majeruhi hayo katika dakika za majeruhi za mchezo huo walioshinda mabao 3-1. Akihojiwa Pellegrini amesema ana imani kabisa kuwa nyota huyo hawezi kukaa nje ya uwanjani kwa msimu wote uliobakia. Meneja huyo aliendelea kudai kuwa kwasasa wanasubiria vipimo lakini madaktari wamemuhakikishia halitakuwa tatizo kubwa.

No comments:

Post a Comment