Wednesday, January 20, 2016

DE GEA HANA MPANGO TENA WA KWENDA MADRID.

GOLIKIPA wa Manchester United David De Gea anaripotiwa kutaka kuendelea kubakia Old Trafford hata kama Real Madrid watarejea kumuwinda tena mwezi huu. Madrid wanatarajiwa kukata rufani adhabu ya kufungiwa kusajili waliyopewa wiki iliyopita lakini kama ikishindikana hawataweza kusajili mchezaji yeyote mpaka kiangazi mwaka 2017. Hata hivyo, bado wana uwezo wa kusajili katika kipindi hiki cha usajili wa Januari na kuna uwezekano wakaanza tena kumfukuzia De Gea. Usajili wa kipa huyo ulishindikana kidogo majira ya kiangazi mwaka jana kutokana na karatasi muhimu kutowasili kwa wakati. De Gea ambaye amesaini mkataba mpya wa miaka minne na United anadaiwa kuwa kwasasa hatoweza kukubali tena kuondoka Old Trafford.

No comments:

Post a Comment