Friday, January 29, 2016

DEMBELE AONGEZA MKATABA SPURS.

MCHEZAJI nyota wa Tottenham Hotspurs, Mousa Dembele ameongeza mkataba wa kuitumikia klabu hiyo na kufuata nyayo za Dele Alli. Toka ametua White Hart Lane Agosti mwaka 2012, Dembele amefanikiwa kuichezea klabu hiyo mechi 143 katika mashindano yote, 20 kati ya hizo ikiwa ni msimu huu. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 28 amesaini mkataba mpya wa miaka mitatu na Spurs ambao utamuweka hapo mpaka mwaka 2019. Akizungumza na mtandao wa klabu hiyo, Dembele alieleza furaha yake kwa kusaini mkataba mpya na kuahidi kufanya kila awezalo kuisaidia timu hiyo kushinda mtaji.

No comments:

Post a Comment