Friday, January 29, 2016

HIDDINK ATHIBITISHA UJIO WA PATO NA MIAZGA.

MENEJA wa Chelsea Guus Hiddink amethibitisha kuwa wanajipanga kumsajili beki wa klabu ya New York Red Bulls, Matt Miazga kabla ya kufungwa kwa dirisha la usajili la Januari. Nyota huyo wa kimataifa wa Marekani alikuwa anapenda kuhamia Ulaya na sasa ataelekea Stamford Bridge pamoja na Red Bulls kuwa wagumu kumuuza chipukizi huyo mwenye miaka 20. Akihojiwa Hiddink amesema Miazgo ni mchezaji mzuri anayechipukia na pamoja kwamba hawatamuharakisha lakini ana imani atafanikiwa kupata namba ya kudumu katika kikosi cha kwanza siku zijazo. Miazga anatarajiwa kujiunga na Chelsea sambamba na Alexandre Pato ambaye Hiddink ameshathibitisha kuwa usajili wake wa mkopo kutoka Corinthians umekamilika.

No comments:

Post a Comment