Sunday, January 31, 2016

TETESI ZA USAJILI ZILIZOJIRI HUKO MAJUU.

KLABU ya Chelsea inaripotiwa kumuwania mshambuliaji wa Atletico Madrid Antoine Griezmann ili aweze kuwa mbadala wa Eden Hazard kama ataondoka majira ya kiangazi.
Chanzo: Daily Mail

KLABU ya Manchester United inatarajia kuwawania nyota wa Tottenham Hotspurs Harry Kane na Dele Alli ambao wamekuwa katika kiwango bora msimu huu.
Chanzo: Express

BEKI wa Paris Saint-Germain Marquinhos anadaiwa kuwindwa na klabu ya Real Madrid ambao wanataka kuimarisha safu yao ya ulinzi kabla ya kufungwa kwa dirisha dogo la usajili na kuanza kutumikia adhabu yao ya kutosajili.
Chanzo: Macca

KLABU ya Newcastle United inaripotiwa kutaka kuimarisha safu yao ya ushambuliaji na wanajipanga kuwafukuzia Seydou Doumbia wa AS Roma na Befetimbi Gomis wa Swansea City.
Chanzo: Le 10 Sport

MSHAMBULIAJI wa Chelsea Lioc Remy anatarajiwa kwenda kwa mkopo Leicester City ambapo inadaiwa kubakia nyaraka chake kabla ya kukamilisha uhamisho huo.
Chanzo: La 10 Sport

KLABU ya Sunderland kwa mara nyingine inataka kumuwania winga Swansea City Andre Ayew majira ya kiangazi baada ya kushindwa kumsajili nyota huyo mwenye umri wa miaka 26 kipindi hiki cha Januari.
Chanzo: Daily Mail

No comments:

Post a Comment