Sunday, January 31, 2016

TERRY KUONDOKA CHELSEA MWISHONI MWA MSIMU.

NAHODHA wa Chelsea John Terry amenyimwa ofa ya mkataba mpya na anatarajiwa kuondoka katika klabu hiyo mwishoni mwa msimu huu.Beki huyo mkongwe mwenye umri wa miaka 35, ambaye amejiunga na klabu hiyo akiwa na umri wa miaka 14, ameshinda mataji manne ya Ligi Kuu, matano ya Kombe la FA na moja la Ligi ya Mabingwa Ulaya akiwa na Chelsea.Akihojiwa Terry amesema angependa kuendelea kubakia lakini inavyoonekana klabu hiyo ina mipango tofauti.Terry pia amesema bado ataendelea kucheza soka lakini sio kwa klabu yeyote ya Uingereza.

No comments:

Post a Comment