Wednesday, January 27, 2016

KIMEELEWEKA, PATO KWENDA CHELSEA.

DEREVA mahiri wa mashindano ya langalanga, Felipe Massa ametuma ujumbe wa kumkaribisha mshambuliaji nyota wa kimataifa wa Brazil, Alexandre Pato katika klabu ya Chelsea. Massa ambaye ana urafiki wa karibu na Pato alituma picha akiwa pamoja na mpenzi wa mwanasoka huyo katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Instagram kumtakia kile la heri rafikiye huyo katika maisha yake mapya Uingereza. Ujumbe huo sasa unathibitisha tetesi zilizozagaa kuwa mshambuliaji anakaribia kukamilisha usajili wake wa mkopo kutoka Corinthians kuwa za kweli. Katika ujumbe wake Massa amesema ana uhakika Pato ataisaidia sana Chelsea hivyo akaipongeza klabu hiyo kwa kupata jembe.

No comments:

Post a Comment