Wednesday, January 27, 2016

RAMIRES AKAMILISHA USAJILI WAKE KWENDA JIANGSU YA CHINA.

KIUNGO wa Chelsea amejiunga rasmi na klabu ya Jiangsu Suning ya China kwa mkataba unaokadiriwa kuwa na thamani ya paundi milioni 25. Nyota huyo wa kimataifa wa Brazil mwenye umri wa miaka 28, alisajiliwa Chelsea akitokea Benfica kwa kitita cha paundi milioni 17 mwaka 2010. Jiangsu walimaliza katika nafasi ya tisa katika msimamo wa Ligi Kuu ya China mwaka jana na wanafundishwa na beki wa zamani wa Chelsea Dan Petrescu. Ramires aliisaidia Chelsea kunyakuwa taji la moja la Ligi Kuu, Kombe la FA, Kombe la Ligi, Ligi ya Mabingwa Ulaya na Europa League.


No comments:

Post a Comment