Wednesday, January 27, 2016

SHAKHTAR DONETSK WANATAKA EURO MILIONI 50 KWA TEIXEIRA.

MENEJA wa Shakhtar Donetsk, Mircea Lucescu anaamini Alex Teixeira anayewindwa na Liverpool ana thamani ya paundi milioni 38. Taarifa zilizosambaa zinadai kuwa Liverpool wanapambana kufikia kiwango ambacho kinatakiwa na Donetsk kwa ajili ya kiungo huyo mwenye umri wa miaka 26. Ofa ya kwanza ya paundi milioni 24 inadaiwa kukataliwa na sasa wanajipanga kutoa nyingine ya pili. Akihojiwa Lucescu amesema Teixeira ni mchezaji bora ambaye anaimarika kila siku hivyo ana uhakika anaweza kufikia kiwango cha Angel Di Maria katika kipindi kifupi kijacho.

No comments:

Post a Comment