Friday, January 22, 2016

KLABU NNE ZINAMFUKUZIA PATO - WAKALA.

WAKALA wa mshambuliaji nyota wa kimataifa wa Brazil, Alexandre Pato amedai kuwa klabu nne ziko katika mbio za kumuwania mteja wake huyo zikiwemo Chelsea na Liverpool. Taarifa zilizozagaa nchini Brazil zimedai kuwa Chelsea tayari wameshafikia makubaliano ya awali juu ya kumchukua Pato katika kipindi hiki cha Januari, ingwa wakala wake Gilmar Veloz amesisitiza hakuna ofa yeyote iliyopelekwa Corinthians. Akihojiwa Veloz amesema amekuw akisikia tetesi nyingi kuhusu mteja wake lakini ukweli ni kuwa hakuna ofa yeyote iliyoopelekwa katika klabu yake. Veloz aliendelea aliendelea kudai kuwa kuna klabu nne za Ulaya zinazomfukuzia Pato nazo ni Chelsea, Liverpool, Sporting Lisbon na Benfica.

No comments:

Post a Comment