Friday, January 22, 2016

SWANSEA YAMRUDISHA TABANOU UFARANSA.

KLABU ya Swansea City imemruhusu Franck Tabanou kujiunga tena na klabu yake ya zamani ya Saint-Etienne kwa mkopo wa mpaka mwishoni mwa msimu huu ikiwa ni miezi saba imepita toka wamsajili beki huyo. Nyota huyo wa kimataifa wa Ufaransa ameshindwa kupata nafasi ya kudumu katika kikosi cha kwanza cha Swansea bada ya kucheza mechi tatu pekee. Tabanou aliisaidia Saint-Etienne kufuzu michuno ya Europa League msimu uliopita lakini ameshindwa kabisa kung’aa katika Ligi Kuu. Akihojiwa Tabanou amesema alikwenda Swansea ili kuimarika zaidi lakini jambo la kushangaza wamekuwa wakimnyima nafasi ya kucheza ndio maana ameamua kurejea katika klabu yake ya zamani.

No comments:

Post a Comment