Friday, January 22, 2016

KLOPP BADO AMNG'ANG'ANIA STURRIDGE.

MENEJA wa Liverpool, Jurgen Klopp amepuuza tetesi zinazomhusisha Daniel Sturridge kuondoka Anfield na kudai atamsubiri mshambuliaji huyo mpaka atakapokuwa fiti. Sturridge amecheza mechi tano pekee za Ligi Kuu msimu huu kutokana na kuandamwa na majeruhi. Hatua hiyo ilipelekea nyota huyo wa kimataifa wa Uingereza kusuhusishwa na tetesi za kuhamia West Ham United wiki hii lakini Klopp amesisitiza kuwa ataendelea kuwa subira kwa mchezaji huyo kadri awezavyo. Klopp amesema ataendelea kumsubiri nyota huyo mpaka atakapopona na wataendelea kumpa msaada wowote atakaohitaji katika kipindi hiki.

No comments:

Post a Comment