Friday, January 22, 2016

MASCHERANO AKWEPA JELA.

BEKI wa Barcelona Javier Mascherano ametoa taarifa inayodai kuwa amefikia makubaliano na mamlaka za Hispania kuhusu kesi yake ya kukwepa kodi. Nyota huyo wa kimataifa wa Argentina alisimama mahakamani ikiwa ni sehemu ya makubaliano ya kukwepa adhabu ya kwenda jela, wakati akisomewa mashitaka mawili ya kukwepa kodi. Hatua hiyo imefikia kufuatia Mascherano kushindwa kuweka wazi mapato aliyopata mwaka 2011 na 2012 ambayo yanakadiriwa kufikia euro milioni 1.5. Taarifa zilizozagaa mapema jana nchini Hispania zilidai kuwa Mascherano alihukumiwa kifungo cha mwaka mmoja jela na kutozwa faini lakini mwenyewe alikanusha tetesi hizo na kudai kuwa wameshafikia makubaliano na wahusika.

No comments:

Post a Comment