Wednesday, January 20, 2016

MAN UNITED YAAMBIWA KUTOA PAUNDI MILIONI 65 KAMA WANAMTAKA LUKAKU.

KLABU ya Manchester United italazimika kulipa kitita cha paundi milioni 65 kama watahitaji kumsajili mshambuliaji wa Everton Romelu Lukaku ambaye yuko katika kiwango bora msimu huu. Lukaku ambaye alisajiliwa Everton akitokea Liverpool kwa kitita cha paundi milioni 28, amefunga mabao 19 katika mshindano yote msimu huu hivyo kuzivutia klabu kubwa zikiwemo Real Madrid, Paris Saint-Germain, Chelsea na Manchester City. Lakini United ndio wanaopewa nafasi kubwa ya kumsajili kutokana na nia yao ya kuimarisha safu yao ya ushambuliaji ambayo imeonekana kuwa butu msimu huu. United imekuwa ikimfuatilia Lukaku kwa karibu msimu huu lakini Everton wamepania kuendelea kubakia na nyota huyo.

No comments:

Post a Comment