Friday, January 22, 2016

MAN UNITED YAKANUSHA KUKUTANA NA GUARDIOLA.

KLABU ya Manchester United imekanusha kuwa wamekutana na meneja wa Bayern Munich Pep Guardiola kuhusu uwezekano way eye kuchukua nafasi ya Louis van Gaal. Mtandao wa France Football umedai kuwa mkutano huo ulifanyika wiki iliyopita jijini Paris lakini United wamesisitiza habari hiyo haina ukweli wowote. Guardiola mwenye umri wa miaka 45 anatarajiwa kuondoka Bayern majira ya kiangazi na amesema tayari ameshapata ofa kadhaa kutoka katika klabu za Uingereza. Klabu ya Manchester City ndio wanaopewa nafasi kubwa ya kumnyakuwa kocha huyo lakini Chelsea na United pia zimekuwa zikihusishwa na tetesi za kumtaka. Bayern walikuwa wameweka kambi yao ya mazoezi huko Doha, Qatar wakati Bundesliga ikiwa katika mapumziko ya majira ya baridi na ligi hiyo inatarajiwa kuendelea tena leo ambapo timu hiyo itakwaana na Hamburg.

No comments:

Post a Comment