Saturday, January 23, 2016

TETESI ZA USAJILI ZILIZOJIRI HUKO MAJUU.

KOCHA Carlo Ancelotti anamtaka Karim Benzema kujiunga na Bayern Munich majira ya kiangazi kama Roberto Lewandowski ataondoka Allianz arena.
Chanzo: OK Dario

MSIMU wa kusuasua alionao Cristiano Ronaldo katika klabu ya Real Madrid umepunguza kasi kwa klabu za Manchester United na Paris saint-Germain kumuwania.United wao wameamua kuhamishia nguvu zao kwa Neymar huku PSG wakitarajiwa kumfukuzia Robert Lewandowski.
Chanzo: Fichajes.net

KLABU za Manchester United na Manchester City zinaripotiwa kupigana vikumbo kumuwania nyota wa Barcelona Neymar kufuatia tetesi za mshambuliaji huyo kutaka kuondoka Camp Nou.
Chanzo: Gazzetta World

KIUNGO wa Chelsea Ramirez anatarajiwa kuondoka kabla ya kufungwa dirisha dogo la usajili kipindi hiki cha Januari huku klabu hiyo ikitarajia kuachia fungu litakalotumika kwa usajili majira ya kiangazi.
Chanzo: Daily Mail

KLABU ya Manchester United imefanya mazungumzo zaidi na Benfica kuhusu nia yao ya kumsajili kiungo chipukizi Renato Sanchez mwenye umri wa miaka 18.
Chanzo: Daily Mail

KLABU ya Liverpool inaripotiwa kuanza mazungumzo na Lorient kwa ajili ya kuwania kumsajili beki wa kushoto Raphael Guerreiro majira ya kiangazi.
Chanzo: calcionews24.com

KLABU ya Borussia Dortmund inataka kumsajili wiga wa Chelsea Bertrand Traore kwa mkopo wa mkpa mwishoni mwa msimu.
Chanzo: Bild

MENEJA wa Bayern Munich Pep Guardiola anatarajiwa kutotangaza uhamisho wake kwenda Manchester City kabla ya kumalizika kwa msimu kwa hofu ya mgongano wa kimslahi kama City watapangwa na Bayern katika ratiba ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Chanzo: The Sun

No comments:

Post a Comment