Monday, January 18, 2016

TETESI ZA USAJILI ZILIZOJIRI HUKO MAJUU.

KLABU ya Manchester United imeripotiwa kuwa wanaweza kumsajili mtoto wa nguli wa zamani wa klabu hiyo Peter Schmeichel aitwaye Kasper kama David De Gea atatimkia Real Madrid majira ya kiangazi.
Chanzo: The Sun

KUFUATIA kuanza msimu kwa kusuasua, Chelsea inaweza kuwakosa nyota wake kadhaa majira ya kiangazi wakiwemo Eden Hazard, Diego Costa, Oscar na Thibaut Courtois.
Chanzo: The Sun

KUFUATIA tetesi za Neymar kufikiria kuondoka Camp Nou baada ya kutumbukizwa katika sakata la usajili wake wakati akitokea Santos, klabu ya Barcelona inajaribu kutafuta mbadala wake kama akiondoka na kuna uwezekano wa kuanza kumuwania Eden Hazard wa Chelsea.
Chanzo: Buzz Sport

KLABU ya Swansea City ina matumaini ya kukamilisha usajili wa Scott Sinclair na mshambuliaji wa AS Roma Seydou Doumbia katika kipindi hiki cha Januari.
Chanzo: The Daily Mail

KLABU ya Newcastle United imeruhusiwa na mmiliki wake Mike Ashley kutumia kiasi cha paundi milioni 100 kipindi hiki cha usajili wa Januari ambapo wamepanga kumuwania Saido Berahino kabla ya kumfukuzia Andros Townsend kutoka Tottenham Hotspurs.
Chanzo: The Daily Mail

KLABU ya Arsenal inajipanga kumuwania mshambuliaji wa Juventus Alvaro Morata katika kipindi ambacho Real Madrid watakuwa wakitumikia adhabu yao ya kufungiwa kusajili, kufuatia tetesi za klabu hiyo kutaka kumrejesha nyota huyo Santiago Bernabeu.
Chanzo: The Sun

No comments:

Post a Comment